Ahueni: Bei ya petroli, dizeli, mafuta ya taa zikishuka
- Bei ya rejareja ya petroli imeshuka kwa Sh187 kwa lita.
- Wakazi wa Dar es Salaam sasa watanunua lita moja kwa Sh2,781 kutoka Sh2,968 ya Machi.
Dar es Salaam.Watumiaji wa vyombo vya moto sasa watakuwa na ahueni baada ya bei za mafuta mwezi Aprili kushuka kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na ilivyokuwa mwezi uliopita.
Bei mpya kikomo zilizotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) zinabainisha kuwa bei ya rejareja ya petroli liyoingizwa kupitia Bandari ya Dar es Salaam imeshuka kwa Sh187, kwa lita huku ile ya dizeli ikipungua kwa Sh284 kwa lita na mafuta ya taa yakipungua kwa Sh169 kwa lita.