Ifahamu mikoa 10 inayoongoza kwa uzazi wa mpango Tanzania

Dar es Salaam. Miongoni mwa masuala yanayogusa zaidi vijana wengi waliopo kwenye ndoa na wasio kwenye ndoa kwa sasa ni suala la kuwa na watoto. 

Miongoni mwa maswali makubwa huwa ni lini wapate watoto, idadi ya watoto lakini ni njia gani sahihi itakayomfanya wanawake vijana wasipate ujauzito bila kutarajia. Wataalamu wanasisitiza kuwa ni vema wazazi vijana wakapanga mipango yao vema ya kijamii na kiuchumi kabla ya kupata watoto. 

Hata hivyo, si watu wote wanapanga ipasavyo juu ya kupata watoto. Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa mwaka 2022 unabainisha kuwa nchini Tanzania takriban wanawake wanne kati ya 10 au asilimia 38 ya waliolewa wenye umri wa miaka 15 hadi 49 wanatumia njia ya aina yeyote ya uzazi wa mpango.

Ripoti ya utafiti huo uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa ushirikiano na taasisi nyingine iwepo Wizara ya Afya inabainisha ipo baadhi ya mikoa yenye kiwango kikubwa cha wanawake wenye wanaotumia ipasavyo njia za uzazi wa mpango ikiongozwa na Njombe huku mingine ikitumia kwa kiwango kidogo sana kama Simiyu. 

Je, waifahamu mikoa inayoongoza kwa matumizi ya njia za uzazi wa mpango Tanzania? 

Ifahamu kansa ya shingo ya kizazi na athari zake

  • Husababishwa na maambukizi ya muda mrefu ya virusi vya  “human papilloma”
  • Virusi hivyo huenezwa kwa njia ya kujamiiana.
  • Upatikanaji duni wa kinga na matibabu huchangia asilimia 90 ya vifo duniani kote.

Dar es Salaam. Licha ya kuwepo nchini kwa miaka mingi kansa ya shingo  ya kizazi imeendelea kugharimu maisha ya wanawake wengi huku kukiwa na uelewa mdogo kuhusu chanzo cha ugonjwa huo na namna unavyoweza kuutibu.

Januari kila mwaka hutumika kutoa elimu na uelewa juu ya visababishi vya ugonjwa huo na jinsi ya kukabiliana nao kwa wasichana.

Taasisi ya Saratani ya Ocean Road inasema kwa kiasi kikubwa saratani hii husababishwa na maambukizi ya mda mrefu (persistence infection) ya virusi viitwavyo “human papilloma”, ambavyo huenezwa kwa njia ya kujamiiana. 

“Kawaida mwili una uwezo wa hudhibiti maambukizi haya yaingiapo mwilini, lakini yasipodhibitiwa kikamilifu na kuwepo mwilini kwa muda mrefu husababisha ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi,” inasema taasisi hiyo.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema matibabu ya mapema yanaweza kuokoa maisha ya wanawake takriban 342,000 waliopoteza maisha kwa ugonjwa huo mwaka 2020 na wagonjwa wapya 604,000 waliopata maambukizi hayo duniani kote kwa mwaka huo huo.

“Knsa ya shingo ya kizazi inazuilika  lakini upatikanaji duni wa kinga, uchunguzi na matibabu huchangia asilimia 90 ya vifo,” linasema Shirika hilo.

Hata hivyo, kabla ya mtu kupata madhara anaweza kugundua mapema dalili za ugonjwa huo kwa kujifanyia uchunguzi mwenyewe.

WHO inasema inachukua miaka 15 hadi 20 kwa saratani ya shingo ya kizazi kukua kwa wanawake walio na kinga ya kawaida na miaka 5 hadi 10 tu kwa wanawake walio na kinga dhaifu, kama vile walio na maambukizo ya VVU ambayo hayajatibiwa.